Pogba Akiri Kufanya Ujinga Man U
KIUNGO wa kati wa Manchester United, Paul Pogba, amekubali kupokea lawama baada ya kucheza rafu dhidi ya mchezaji wa Arsenal, iliyosababisha penati ambayo iliamua matokeo ya mchezo huo wa ligi kuu ya England.
Pogba alinyanyua mguu uliomuangusha Hector Bellerin ndani ya eneo la hatari na Pierre-Emerick Aubameyang akafunga bao lililoipa ushindi The Gunners.
”Tunajua kwamba kilikuwa ni kiwango duni, mimi binafsi sikupaswa kucheza rafu ya aina ile. Nilidhani ningeugusa mpira lakini sikufanya hivyo. Sikupaswa kutoa adhabu mbaya kama hiyo,” amesema Pogba.