STAA wa soka Paul Pogba ameiambia timu yake ya Manchester United kwamba anataka kuondoka na kujiunga na Barcelona. Amewaambia wachezaji na maofisa wa klabu hiyo kwamba anataka kuuzwa, miaka miwili baada ya kujiunga na timu hiyo akitokea Juventus ambapo timu yake ya sasa ilimnunua kwa kitita kilichovunja rekodi ya dunia cha Paundi mil. 89 (Sh. 262 bilioni).
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25, amemtumia pia ujumbe Ed Woodward, mwenyekiti mtendaji wa Man U, akimweleza nia yake ya kuondoka.
Comments are closed.