Polisi Mwanza ‘Walivyoua’ Majambazi 8, RPC Afunguka – VIDEO
Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza limefanikiwa kuwaua majambazi nane wilayani Ukerewe Mwanza baada ya kupambana na majambazi hao huku wawili wakisadikika kutoroka.
Tukio hilo limetokea Usiku wa kuamkia leo Jumamosi katika Visiwa vya Ukerewe Mwanza
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Jonathan Shana ametoa wito kwa jamii kujiepusha na vitendo vya uhalifu kwani Jeshi hilo limejipanga kukabiliana na watu wanaofanya uhalifu katika kila eneo la Mkoa wa Mwanza.
Comments are closed.