The House of Favourite Newspapers

Polisi Warushiana Risasi na Majambazi Waliovamia Sheli, Mmoja Auawa

0
Polisi wamefanikiwa kuwadhibiti majambazi waliotaka kutekeleza uhalifu katika Seli ya Benaco

JESHI la Polisi Mkoa wa Kagera limefanikiwa kuzuia tukio la ujambazi wa kutumia silaha lililokuwa linapangwa na majambazi watatu waliokuwa wanajaribu kuvamia kituo cha mafuta (petrol station) cha Benaco Oil kilichopo Benako Wilaya ya Ngara mkoani humo.

Bunduki iliyokamatwa wakati wa mapigano kati ya Jeshi la Polisi na Majambazi

Kamanda Mkuu wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kagera William Mwampaghale amesema tukio ilo lilitokea tarehe 7/12/2022 majira ya saa 2:30 usiku katika kijiji cha Rwakalemela kata ya Kasuro wilaya humo,ambapo majambazi watatu walirushiana risasi na polisi majambazi wawili walikamatwa mmoja kati hao alifariki wakati akikimbizwa hospitalini uku jambazi mmoja akifanikiwa kutoroka.

Leave A Reply