The House of Favourite Newspapers

PSG Waweka Ngumu Kwa Mbappe

0

PSG imezidi kuipa wakati mgumu Real Madrid baada ya kukataa ofa yao ya pili kwa ajili ya kumuachia Kylian Mbappe
na sasa wanasubiri ofa ya tatu.


Awali Madrid iliwasili-sha ofa ya pauni 137m ambayo ilikataliwa, huku mara ya pili wakiweka pauni 154, nayo imekataliwa.
Madrid imekomalia dili la Mbappe kutua ndani ya Santiago Bernabeu, huku mchezaji mwenyewe akitaka kuondoka ndani ya timu hiyo ndiyo maana amekataa kusaini mktaba mpya.


Kwa sasa Madrid wa-najipanga upya kwa ajili ya kuwasilisha ofa ya tatu na kama watashind-wa hapo basi watasubiri hadi Januari,     mwakani.

WALICHOKIFANYA MASHABIKI WA YANGA MANYARA KUELEKEA KILELE cha WIKI ya MWANANCHI.

Leave A Reply