The House of Favourite Newspapers

PSSSF Yaanika Mikakati Kuwalipa Wastaafu

Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Uma wa PSSSF, Eunice Chiume akisaini kwenye kitabu cha wageni katika Ofisi za Global Group.

Uongozi wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), umetembelea ofisi za Global Group zilizopo Sinza Mori kwa ajili ya kutoa Elimu kwa wananchi juu ya Huduma zitolewazo na Mfuko huo.

Eunice Chiume akizungumza na Mkurugenzi Mtendaji wa Global group, Eric Shigongo.
Akizungumza na +255 Global Radio Meneja Kiongozi Uhusiano na Elimu kwa Uma PSSSF, Eunice Chiume amesema utaratibu ni kufanya uhakiki kila mwaka kwa wastaafu wa mfuko huo.
Ofisa uhusiano Mwandamizi wa PSSSF, Abdul Njaidi akisaini.
PSSSF Imeundwa kupitia Mifuko ya Pensheni minne ambayo ni Mifuko ya PSPF, LAPF, PPF na GEPF na kuunda Mfuko mmoja kwa ajili ya Watumishi wa Umma unaojulikana kama Mfuko wa Hifadhi kwa Watumishi wa Umma.
Mhariri wa Gazeti la Ijumaa, Sifael Paul akimwonyesha gazeti Eunice.
Mhariri wa Gazeti la Uwazi, Elvan Stambuli akisalimiana na Eunice.
Mhariri wa gazeti la Championi, John Joseph akimwonyesha gazeti hilo.
Mwandishi wa Championi, Omary Mdose akimwonyesha Gazeti la Betika.
Mwandishi Martha Mboma akimkabidhi gazeti la Spoti Xtra.
Mkuu wa Idara ya Digital, edwin Lindege akitoa maelezo kwa Eunice namna wanavyoandaa habari na kuzifikisha kwa jamii kupitia njia ya mitandao (Online Digital Platforms).
Mkuu wa Idara ya Global TV, Abdallah Ng’anzi akitoa maelezo namna ambavyo timu yake inafanya kazi.
Kutoka kushoto ni Mhariri Mtendaji wa Global Publishers, Saleh Ally, Eunice, Meneja Mkuu, Abdallah Mrisho na Njaidi ndani ya studio za Global TV Online.
Eunice na Njaidi ndani ya Studio za Global Radio.
Eunice akifanya mahojiano na +255 Global Radio.
PICHA: MUSA MATEJA | GPL

Comments are closed.