



Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi, amekutana na uongozi wa Benki ya NMB Ikulu Jijini Zanzibar na kueleza kuwa yupo tayari kushirikiana na Benki hiyo kwa ajili ya kuimarisha uchumi pamoja na huduma za kijamii Zanzibar.
Rais Dk. Hussein amesema kuwa Benki ya NMB imepata mafanikio makubwa hivyo, Serikali anayoiongoza iko tayari kushirikiana na NMB katika kuimarisha miradi mbalimbali ya kiuchumi.

