Rais mstaafu Dkt. Kikwete Awasilisha Ujumbe Maalum nchini Senegal
Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete Machi 24, 2025, amewasilisha Ujumbe Maalum wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Rais wa Jamhuri ya Senegal, Bassirou Diomaye Faye katika Ikulu ya Rais huyo jijini Dakar, Senegal.