The House of Favourite Newspapers

Rais Mstaafu Kikwete na Mkewe Wafika nyumbani kwa Hayati Ali Hassan Mwinyi kutoa pole kwa familia-Video


Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi akiwa Mikocheni nyumbani kwa baba yake akiendelea kupokea mkono wa pole kutoka kwa Rais Mstaafu Jamhuri ya Muungano wa Tanzania  Jakaya Mrisho Kikwete na viongozi, ndugu, jamaa na marafiki kufuatia kifo cha Rais Mstaafu Mzee Ali Hassan Mwinyi kilichotokea jana tarehe: 29 Februari 2024.

Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa na mkewe ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga, Salma Kikwete wakiwa nyumbani kwa Rais Mstaafu, Hayati Ali Hassan Mwinyi, Mikocheni mkoani Dar es Salaam kutoa pole kwa familia kufuatia kifo cha kiongozi huyo.

Rais Mstaafu, Dkt. Jakaya Kikwete akiwa na mkewe ambaye pia ni Mbunge wa Mchinga, Salma Kikwete leo Machi 1, 2024 wamefika nyumbani kwa Rais Mstaafu, Hayati Ali Hassan Mwinyi, Mikocheni mkoani Dar es Salaam kutoa pole kwa familia kufuatia kifo cha kiongozi huyo.