The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Afuatilia Uwasilishaji wa Bajeti Kuu ya Serikali 2025/26 – Video

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akifuatilia Bajeti Kuu ya Serikali ya mwaka 2025/26 iliyokuwa ikisomwa Bungeni na Waziri wa Fedha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba. Rais Dkt. Samia alikuwa akifuatilia Bajeti hiyo kwa njia ya Runinga kupitia Televisheni ya Taifa (TBC1) Ikulu Chamwino, Mkoani Dodoma tarehe 12 Juni, 2025. Bajeti Kuu ya Serikali imesomwa katika Bunge la 12, mkutano wa 19 kikao cha 45 Jijini Dodoma.

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Tulia Ackson amelitangazia bunge kuwa Rais Samia Suluhu Hassan atakuwa akifuatilia kwa njia ya runinga bajeti kuu ya serikali inayosomwa bungeni na Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba.