The House of Favourite Newspapers
gunners X

Rais Samia Akemea Uzembe wa Posho kwa Wachezaji Taifa Stars – ( Picha + Video)

0
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,  Dkt. Samia Suluhu Hassan, akizungumza na wanamichezo mbalimbali, Ikulu Jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya kuwapongeza mara baada ya kufanya vizuri katika mashindano ya kimataifa, tarehe 10 Januari 2026.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amesema alishtushwa na taarifa za wachezaji wa Timu ya Taifa (Taifa Stars) kudai kugoma kusafiri kwenda Morocco kabla ya Fainali za AFCON 2025, wakilalamikia posho zao.

Akizungumza Januari 10, 2026 katika hafla ya kuipongeza Taifa Stars kwa mafanikio yao, Rais Samia amesema taarifa hizo hakuzipokea kwa namna nzuri, hata hivyo alifarijika kuona kuwa mgomo huo haukufanyika.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea zawadi ya jezi ya Timu ya Taifa ya mpira wa miguu ya wanaume ‘Taifa Stars’ iliyosainiwa na wachezaji kutoka kwa nahodha msaidizi wa timu hiyo, Bakari Nondo Mamnyeto, kwenye hafla ya kuwapongeza iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 10 Januari 2026.

“Jicho letu liwe kwa vijana wetu. Kuwafanyisha mazoezi ni muhimu, lakini pia kuzingatia maslahi yao. Kuna siku nilikuwa nimekaa, mara paap napokea taarifa kutoka vyombo vyangu vya serikali kwamba wachezaji wamegoma kwenda Morocco kutoka Misri.

“Nikasema nini? Kiposho kidogo hakitoshi? Mungu wangu wee! Nikamwita Makonda (Paul) nikamuuliza haya mnafanyaje kuhusu hili? Sitaki vijana wetu wawe wameshuka morali kwa namna yoyote, ebu changamka basi,” amesema Rais Samia.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, akipokea tuzo kutoka kwa Rais wa Shirikisho la Soka Barani Afrika (CAF), Dkt. Patrice Motsepe, iliyokabidhiwa kwake na aliyekuwa Waziri wa Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo, ambaye kwa sasa ni Waziri Mteule wa Nchi, Ofisi ya Rais, Ikulu (Kazi Maalum), Profesa Palamagamba Kabudi, wakati wa hafla ya kuwapongeza wanamichezo waliofanya vizuri katika mashindano ya kimataifa, Ikulu Jijini Dar es Salaam, tarehe 10 Januari 2026. Rais Mhe. Dkt. Samia amekabidhiwa tuzo hiyo kutokana na kutambua mchango wa Serikali katika kukuza mchezo wa mpira wa miguu Barani Afrika.

Rais Samia ameongeza kuwa alifurahishwa na hatua ya Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda, alipotangaza dau la shilingi milioni 200 kwa timu hiyo, hatua aliyosema ilisaidia kurejesha morali ya wachezaji.

“Mara paap namsikia Makonda anatangaza dau la milioni 200, nikasema yes, hivyohivyo,” ameongeza.

Aidha, Rais Samia amesisitiza kuwa serikali itaendelea kujitahidi kuhakikisha wachezaji wa Taifa Stars wanapata stahiki zao kwa wakati ili kuwawezesha kuwakilisha taifa kwa morali na ari ya juu.

Leave A Reply