The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Amuapisha CP Jeremiah kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Kamishna Jenerali wa Magereza (CGP) Jeremiah Yoram Katungu kuwa Mkuu wa Jeshi hilo kwenye hafla iliyofanyika Ikulu Jijini Dar es salaam tarehe 31 Julai, 2024.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Julai 31, 2024 amemuapisha CP Jeremiah Yoram Katungu kuwa Kamishna Jenerali wa Jeshi la Magereza. Hafla hiyo imefanyika Ikulu,jijini Dar es Salaam.