The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Apokea Tuzo Ya Gates Goalkeeper Award, Hyatt Regency – (Picha+Video)

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akihutubia viongozi mbalimbali kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo Maalum ya Kimataifa ya The Global Goalkeeper Award iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Februari, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan Akipokea Tuzo ya Gates Goalkeeper Awards Hyatt Regency Hotel Dar es salaam, leo tarehe 04 Februali, 2025.

Rais Samia Suluhu Hassan, amekupokea tuzo ya hiyo ikiwa ni kielelezo cha matokeo makubwa ambayo yamepatikana katika uongozi wake kufuatia ripoti ya utafiti wa demografia na afya ya mwaka 2022 inayoonesha kupungua kwa vifo vitokanavyo na uzazi kwa kiwango cha asilimia 80 pamoja na watoto wachanga.

Tuzo hiyo hutolewa kwa viongozi waliowezesha nchi zao kuharakisha maendeleo kuelekea kufikia malengo ya maendeleo endelevu.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan akipokea Tuzo Maalum ya Kimataifa ya The Global Goalkeeper Award kutoka kwa Rais wa Kitengo cha Usawa wa Jinsia kutoka Taasisi ya Gates, Dkt. Anita Zaidi kwenye hafla iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Februari, 2025.
Rais Samia amepokea Tuzo Maalum ya Kimataifa ya The Global Goalkeeper Award
Rais Samia akiwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Philip Isdor Mpango, Rais wa Kitengo cha Usawa wa Jinsia kutoka Taasisi ya Gates kutoka Marekani Dkt. Anita Zaidi, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Tulia Ackson, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Afya Mhe. Jenista Mhagama, Rais Mstaafu wa Zanzibar Dkt. Amani Abeid Karume na Viongozi mbalimbali kwenye hafla ya utoaji wa Tuzo ya Kimataifa ya The Global Goalkeepers Award kutoka Taasisi ya Gates ya Marekani. Hafla hiyo ilifanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Jijini Dar es Salaam tarehe 04 Februari, 2025.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye mazungumzo na Rais wa Kitengo cha Usawa wa Jinsia kutoka Taasisi ya Gates Dkt. Anita Zaidi katika Hoteli ya Hy