The House of Favourite Newspapers

Rais Samia Ashiriki maadhimisho ya miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi Dodoma (Picha +Video)


Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wanachama wa CCM.

Rais Samia Suluhu Hassan amempongeza Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Stephen Wasira, na kueleza kuwa amethibitisha kwamba mkutano mkuu haukukosea kumpitisha kwa kura nyingi.

Rais Samia ameyasema hayo leo wakati akihutubia kwenye sherehe za maadhimisho ya miaka 48 ya Chama cha Mapinduzi yanayofanyika jijini Dodoma.

Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi na Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan akisalimiana na wanachama, wakereketwa na wapenzi wa Chama Cha Mapinduzi katika sherehe za maadhimisho ya Miaka 48 ya Kuzaliwa kwa CCM leo 05 Februari 2025 uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma
Katibu Mkuu wa CCM na Mgombea Mwenza Mteule wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa Tiketi ya CCM Dkt. Emmanuel Nchimbi akizungumza na Wanachama, Wakereketwa na Wafuasi wa Chama Cha Mapinduzi waliohudhuria sherehe za maadhimisho ya Kuzaliwa kwa CCM ; Jamhuri Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt. Hussein Ali Mwinyi akishiriki kilele cha Maadhimisho ya Miaka 48 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi katika uwanja wa Jamhuri Jijini Dodoma tarehe 5 Februari 2025.