Rais Trump Aondoka Ikulu na Mkewe Melania (Picha +Video)
RAIS Donald Trump ameondoka Ikulu ya Marekani leo Januari 20, 2021 akiwa na mkewe saa 2:12 asubuhi (Tanzania ilikuwa saa kumi jioni leo) ambapo alizungumza na waandishi wa habari akisema kuwa rais wa nchi hiyo ilikuwa ni ‘heshima ya maisha’.
Akiwa katika kituo cha kijeshi cha Andrews, aliwaambia waandishi wa habari kwamba atarejea ‘kinamna’ na aliwaambia wote waliokuwepo: “Muwe na maisha mema”.
Wakiwa eneo la Mar-a-Lago, Trump na familia yake watatazama kuapishwa kwa rais mteule, Joe Biden, akiwa rais wa 46 wa Marekani.