Ratiba ya Kufuzu AFCON Yatoka, Taifa Stars na Uganda Zapangwa Kundi Moja
MAKUNDI ya kufuzu fainali za mataifa ya Afrika AFCON imetoka ambapo timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars imeangukia kwenye kundi F ambalo linashirikisha mataifa ya Uganda, Niger pamoja na Algeria.
Bingwa mtetezi, timu ya taifa ya Senegal itaanza harakati za kutetea kombe lake katika kundi L ambalo linashirikisha timu za Jamhuri ya Benin, Rwanda pamoja na Msumbiji.
Mwenyeji wa Mashindano timu ya taifa ya Ivory Coast imepangwa kundi H na timu za taifa za Zambia, Comoro pamoja na Lesotho.
Mashindano hayo yanatarajiwa kufanyika nchini Ivory Coast mwakani ambapo hadi sasa maandalizi yanaendela vizuri ikiwa ni pamoja na uandaaji wa viwanja pamoja na miundombinu mingine.