RC Makonda: Tulieni Polisi Wanafanyia Kazi Utekaji wa Mo Dewji
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, amewaomba wakazi wa Dar es Salaam kutulia wakati huu kuhusu kutekwa mfanyabiashara na mwekezaji katika Klabu ya Simba, Mohammed Dewji (Mo Dewji) kwani jeshi la polisi tayari limeshaanza uchunguzi na limebaini watekaji ni Wazungu raia wa nchi za nje. Hivyo kila mmoja kwa nafasi yake ashiriki kutoa taarifa za utekwaji wa mtu huyo uliofanyika katika gym ya Hoteli ya Colosseum, Oyster Bay jijini Dar es Salaam alfajiri ya leo, ili kurahisisha kazi ya polisi.
PICHA/HABARI: MUSA MATEJA | GPL
Comments are closed.