The House of Favourite Newspapers

REAL MADRID YAMRUDIA TENA DAVID DE GEA

0
Kipa wa Manchester United, David de Gea.

Real Madrid imerejesha mipango yake ya kumuwania kipa David de Gea kutoka Manchester United kabla ya dirisha la usajili kufungwa.

Kocha wa Real Madrid, Zinedine Zidane amefikia uamuzi huo bada ya kukosa matumaini ya kumsajili Kylian Mbappe kutoka Monaco.

De Gea ilibaki kidogo ajiunge na Madrid mwaka 2015 kabla ya kushindikana dakika za mwisho kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.

Hata hivyo, bado Man United haijatoa kauli ya mwisho kuhusu harakati hizo za Madrid kwa De Gea huku yenyewe ikiwa inamuwania Thomas Lemar kutoka Monaco na imeweka dau la pauni milioni 55 mezani.

 

Usipitwe na Matukio, Install ===>Global Publishers App

VIDEO: Vilio Tena Shule ya Lucky Vincent, Arusha (VIDEO)

Leave A Reply