The House of Favourite Newspapers

Redondo Amewaka Kweli Kweli

0

KIUNGO wa Biashara United Ramadhan Chombo (Redondo), Jumamosi iliyopita alionyesha kiwango cha juu baada ya kufunga mabao mawili wakati timu yake ya Biashara ilipowachapa FC Dikhil ya Djibout mabao 2-0.

 

Mbali na kufunga mabao hayo, kiungo huyo wa zamani wa Simba ameingia kwenye kitabu cha kuwa mchezaji wa kwanza wa Biashara United kufunga mabao mawili na kukosa penalti kwenye mchezo mmoja wa kimataifa.

 

Rekodi ambaye ni mchezaji wa zamani wa Simba alionyesha kiwango hicho kwenye mchezo wa marudiano wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi FC Dikhil ya Djibout na kwenda hatua inayofuata kwa jumla ya mabao 3-0. Kwenye mechi hiyo Redondo alikosa pia na penalti.

ISSA LIPONDA, Dar es Salaam

Leave A Reply