The House of Favourite Newspapers

Rekodi… Yanga Ilivyoipoteza Simba Ngao ya Jamii

0

 

Yanga.

UHONDO wa Ngao ya Jamii kati ya Yanga na Simba ni keshokutwa Juma­tano. Hii itakuwa ni mechi ya nne timu hizo kuku­tana katika mi­chuano hiyo lakini mechi hii inatara­jiwa kuwa kivu­tio kikubwa zaidi kutokana na usa­jili ulivyofanyika.

Michuano hii ya Ngao ya Jamii, kwa kawaida huwa ni ‘Super Cup’, kwa maana ya kukutani­sha mabingwa wa michuano miwili to­fauti (au bingwa wa FA vs mshindi wa pili wa ligi kama bingwa wa ligi na FA ni yuley­ule) lakini kwa muda mrefu kwa Bongo imekuwa ikimku­tanisha mshindi wa kwanza na wa pili wa ligi kuu kwa kuwa hatukuwa na Kombe la FA, hivyo kukosa mantiki.

Safari hii kuna uhalisia zaidi, watu wataona nani mkali kati ya bingwa wa ligi kuu (Yanga) na wa Kombe la FA (Simba). Kwa Tanzania, hii ni itakuwa ni mechi ya 10 ya Ngao ya Jamii, tangu ilivyoan­zishwa mwaka 2001, kisha ikafa na kuja kuibuka tena baada ya miaka nane.

YANGA YACHE­ZA MARA NY­INGI ZAIDI YA SIMBA

Yanga ndiyo timu ambayo imecheza mechi nyingi zaidi za Ngao ya Jamii tangu ilivyoanzishwa mwa­ka 2001 kati ya timu nne ambazo zime­wahi kucheza mechi hiyo.

Hadi sasa ina jumla ya mechi nane ambazo imecheza dhidi ya Simba mara (3), Mtibwa mara (1) na Azam mara (4).

Simba imecheza michuano hii mara nne dhidi ya Yanga mara (3) na dhidi ya Azam mara (1). Azam wamecheza mara tano mfululizo kuanzia 2012, dhidi ya Simba mara (1) na dhidi ya Yanga mara (4). Mtibwa ni mara moja dhidi ya Yanga.

YANGA YAT­WAA NGAO 5, SIMBA 2

Yanga imefaniki­wa kutwaa Ngao ya Jamii mara tano zaidi ya Simba ambayo imechukua mara mbili tangu ilipoanza kushiriki.

 

Simba.

YANGA 5, SIM­BA 4

Yanga imefani kiwa kui­funga Simba jumla ya mabao matano katika Ngao ya Jamii pindi ili­pokutana katika miaka tofauti ambapo mwaka 2001, Wa­najangwani hao waliibuka na ush­indi wa mabao 2-1 na mwaka 2010 waliifunga penalti 3-1. Lakini Simba imewafunga wapinzani wao hao jumla ya ma­bao manne yakiwemo mawili kwenye ushindi wa 2-0 mwaka 2011.

WAFUNGAJI SIM­BA, YANGA ZILI­VYOKUTANA

Yanga 2-1 Simba (2001)

Mabao ya Yanga yali­fungwa na Edibily Lunyam­ila na Ally Yusuph ‘Tigana’ la Simba lilifungwa na Steven Ma­punda.

Simba 1-3 Yanga (2010) penalti

Penalti ya Simba ilifungwa na Mohamed Banka huku Emmanuel Okwi na Uhuru Seleman wakikosa penalty, na kwa upande wa Yanga zilipigwa na Godfrey Bonny, Stephano Mwasyika na Isack Boakye.

Simba 2- 0 Yanga (2011)

Wafungaji Haruna Moshi ‘Boban na Felix Sunzu.

AZAM MECHI 5, IME­CHUKUA MA R A MOJA

Azam ndiyo timu yenye historia ya kucheza Ngao ya Jamii mara nyingi zaidi na kushindwa kuchukua kombe hilo . Azam wa­mecheza mara tano kwenye mechi hizo na ku­fanikiwa kushinda mara moja pekee.

M T I B W A SUGAR NAO WAMO

Mtibwa Sugar ya Morogoro nayo iliwahi kuonja raha ya ushindi wa mchezo huu, kwani iliifunga Yan­ga bao 1-0 mwaka 2009.

Khadija Mngwai na Ibrahim Mressy

 

Baada ya Lissu Kuliamsha Dude, Serikali Yafunguka Sakata la Bombadier

Usipitwe na Matukio, Install ===>Global Publishers App

Sikiliza Hadithi za Mtunzi Eric Shigongo Hapa

Leave A Reply