The House of Favourite Newspapers

Rich Mavoko Ashinda Kesi Dhidi ya WCB

EXCLUSIVE: Msanii Rich Mavoko ameshinda kesi ya kujiengua katika Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB). Kesi hiyo ilikuwa ikisikilizwa katika Ofisi za Baraza la Sanaa Tanzania (Basata).

Takribani miezi miwili iliyopita taarifa zilianza kusambaa kuwa Mavoko ametimuliwa WCB huku nyingine zikieleza kuwa amejiengua mwenyewe.

Aidha, viongozi wa lebo hiyo hawajataka kuweka bayana kinachoendelea dhidi ya Mavoko ambapo hivi karibuni, Mmoja wa viongozi hao, Hamis Taletale ‘Babu Tale’ hivi karibuni alikaririwa akisema wakati wa kuzungumzia jambo hilo haujawadia.

Taarifa zaidi endelea kufuatilia mitandao ya Global Publishers.

Comments are closed.