The House of Favourite Newspapers

Rihanna Beyonce, Kuunganishwa Na Bendi!

0

rihana and beyonceRobin Rihanna Fenty ‘Rihanna’ (kushoto) na Beyonce Knowles ‘Beyonce’.

Na Hamida Hassan

HOUSTON, Marekani

KUNA madai kuwa mastaa wawili mahasimu, Robin Rihanna Fenty na Beyonce Knowles wako katika mazungumzo na waandaaji wa shoo ya Super Bowl ili wakikubaliana wafanye shoo angalau kwa nusu saa.

Taarifa iliyoripotiwa na Gazeti la Mirror imeeleza kuwa, mdau mmoja aliyefahamika kwa jina la Chris Matin amefanya mazungumzo maalum na wasanii wote wawili kwa ajili ya shoo hiyo.

“Chris na bendi yake wanatarajia kuwa na wasanii kama Katy Perry na Madonna pamoja na wacheza shoo wake lakini wameamua kuwashawishi wasanii hao ili kuwa na ‘sapraizi’ tofauti siku hiyo,” ilielezwa.

Kama Chris atakuwa amefanikiwa kuwaunganisha mastaa hawa atakuwa amefanya kitu kikubwa kwani wamekuwa kwenye bifu la muda mrefu.

Leave A Reply