The House of Favourite Newspapers

Robo Fainali Ya EFL Cup: Arsenal vs Man City, Everton vs Man United, Hapatoshi!!!

0

Mwezi Disemba ni mwezi wenye burudani kwa mashabiki wa soka. Kunako Ligi Soka ya Uingereza, robo fainali ya EFL Cup kutimua vumbi wiki hii.

Arsenal kuwakaribisha Manchester City katika dimba la Emirates Jumanne hii. Huu ni mchezo wa 202 kwa timu hizi kukutana katika historia ya soka.

 

Kabla ya mchezo huu, Arsenal ameshawafunga City mara 98, wametoka sare mara 45 na City ameibuka kidedea mara 58. Katika michezo 5 ya mwisho kwa Arsenal na Man City kukutana, City ameshinda mara 4 na kapoteza mara 1.

 

Pep Guardiola atalipa kisasi kwa Mikel Arteta baada ya kupoteza mchezo wa fainali ya FA Cup, au Arteta ataendeleza ubabe kwenye Carabao Cup?

 

Upande wa pili kutakuwa na vita nyingine ambapo Carlo Ancelotti atamkaribisha Ole Gunnar Solskjaer pale Goodison Park.

Everton na Manchester United watakutana kwa mara ya 205 katika historia ya soka nchini Uingereza. Takwimu zinaonesha, kuelekea mchezo huu – United ameshinda michezo 89, amepoteza michezo 70 na wametoka sare mara 45.

 

Katika michezo 10 ya mwisho kwa timu hizi kukutana kwenye mashindano yote, United ameshinda mara 5, wametoka sare mara 4 na Everton ameshinda mara 1.

 

Hii ni michezo ya hatua ya robo fainali kwenye EFL Cup . Yeyote atakayepoteza mchezo huu atayaaga mashindano. Je ni Ole, Ancelotti, Guardiola au Arteta atakayeibuka kidedea au pengine kufungasha virago msimu huu?

 

Mchongo mzima upo kwa Wataalamu wa Meridian, odds za kibingwa kwa michezo hii na mingine mingi ipo hapa.

Jisajili na Meridiabet hapa http://www.meridianbet.co.tz na furaha yako itaanzia hapo.

 

Pakua App ya Meridianbet kwenye simu yako na uanze kubashiri kwa uhuru nyumbani kwako. Pia, unaweza kuweka pesa kwenye akaunti yako kupitia KwikPay, M-PESA au Airtel Money. Kumbuka, daima hauwezi kupoteza tiketi yako ya kwanza ukiwa na Meridianbet, tuna Bonasi ya 100% inakusubiri.

 

Meridian – Nyumba yenye odds bora na bonasi kubwa!

 

Leave A Reply