ROMA KUWAKALISHA RAIS MAGUFULI NA LOWASSA SITI MOJA
Staa wa ngoma ya Zimbabwe ambayo ndiyo homa ya jiji kwa sasa, Ibrahim Mussa ‘Roma Mkatoliki’, amesema kuwa ikitokea amepanda daladala ambayo ndani yake kuna siti moja tu iliyo wazi nyingine zote zimejaa, halafu Rais Magufuli na Lowassa wamesimama, atakachokifanya ni kufosi wote wakae, na siyo kumpisha mmoja wapo.
Roma aliyasema hayo, alipokuwa nchini Kenya, kwenye mahojiano maalum aliyofanya na Redio Maisha, ambapo walimuuliza swali hilo na hayo ndiyo yalikuwa majibu yake.
NA ISRI MOHAMED/GPL