Bondia Baina Mazola na Sadiki Momba usiku wa kuamkia leo walitoana kijasho ulingoni kwenye mpambano wa raundi nane usiokuwa wa ubingwa uliopigwa Uwanja wa Kinesi uliopo Ubungo Shekilango Dar.
Katika pambano hilo mabondia hao walichapana vyakutosha kila mmoja akitumia maelekezo ya mwalimu wake lakini mwisho wa yote mwamuzi wa pambano hilo alitangaza matokeo ya sare.
Kama ulivyo kawaida yake mchezo wa ngumi matokeo hayo yalizua zogo kila mmoja akimtaja bondia anayemshabikia kuwa ndiye mshindi.
Mabondia hao walipohojiwa na wanahabari kila mmoja alijitapa kushinda pambano hilo na kuzidi kumtambia mwenzake hivyo kutengeneza mazingira ya kurudiwa siku nyingine.
HABARI/PICHA ZOTE NA RICHARD BUKOS /GPL
Angalia picha