Sakina Lyoka asherehekea ‘bethidei’ yake na Mashauzi Classic
Mtangazaji wa Clouds TV, Sakina Lyoka (kushoto), akisaidiana kukata keki na mama yake mzazi.
Sakina akimlisha keki mama yake mzazi.
Mama Sakina akimlisha keki mwanaye.
Profesa Lyoka, baba mzazi wa Sakina, akilishwa keki na mwanaye.
Sakina akimtunza mama yake fedha muda mfupi baada ya kundi la Mashauzi Classic kupiga wimbo wa Mama Nipe Radhi na kuinuka kucheza wimbo huo.
Msanii wa Bongo Fleva, Tunda Man, akilishwa keki.
Keki ya sherehe ikiwa mezani kabla ya kukatwa.
MTANGAZAJI wa kipindi cha Ng’aring’ari kinachorushwa hewani kupitia Clouds TV, Sakina Lyoka, usiku wa kuamkia leo alisherehekea siku ya kuzaliwa kwake ndani ya Ukumbi wa Mango Garden, Kinondoni, huku bendi ya Mashauzi Classic ikitumbuiza.