The House of Favourite Newspapers

Saluni Hii ‘Balaa’ kwa Urembo, Mitindo Dar; Tazama Wanachokifanya – VIDEO

KAMA wewe ni dada au mama unayekiumiza kichwa chako kutafuta saluni itakayokuremba na kukufanya uonekane mrembo bila kuathiri ngozi yako au nywele zako, jibu ni moja tu, wacheki Goddess Glam Salon.  Hapa kuna kila huduma ya urembo unayoifahamu.
Kuanzia leo achana na saluni bubu zisizoeleweka ili  zisikuharibie mvuto wako bure.  Goddess Glam Salon nd’o saluni  pekee inayokufaa, ni saluni ya wanawake ya kiwango cha juu, iliyopo Kinondoni Biafra jijini Dar es Salaam, mkabala na Kanisa la Tanzania Assemblies of God (TAG).

Goddess Glam Salon ina mandhari safi ya kukufanya ufurahie muda wote unapopata huduma yetu; tuna watalaam waliosomea na kubobea katika masuala ya urembo wa ngozi, nywele, kucha na mapambo. Tunawathamini na kuwajali sana wateja wetu ili kuwapa kile wanachokihitaji.

Katika msimu huu ambapo tunaelekea kwenye sikukuu za mwisho wa mwaka, Goddess Glam Salon tumekuletea ofa kabambe ambao ni:

Maharusi wote wanaotarajia kufunga ndoa mwisho wa mwaka huu (2018), tunatoa punguzo la asilimia 75 yaani bei sawa na bure huku ukipatiwa huduma zote stahiki, make-ups, manicure, pedicure, styles tofauti za nywele bila kusahau massage ya mwili mzima.

Kwa wasio maharusi pia wanapata punguzo la asilimia 50 kwa huduma za kusuka, makeups, kucha, pamoja na kubana mitindo yote. Ukija na familia yako pia utapata punguzo la asilimia 50.
Kwa mawasiliano zaidi tupigie kwa namba; +255 715 787876.
Wote mnakaribishwa!

Salon Hii ni Balaa kwa Dar} VIDEO

Comments are closed.