The House of Favourite Newspapers

Samatta Ajiunga Na Fenerbahce Ya Uturuki

0

MSHAMBULIAJI wa timu ya soka nchini Tanzania Mbwana Samatta leo Septemba 25, 2020 amejiunga na klabu ya Uturuki Fenerbahce kwa mkataba wa miaka minne.

Samatta alikuwa anakipiga ndani ya Aston Villa inayoshiriki Ligi Kuu England, ila kwa msimu wa 2020/21 alikwama kupenya kikosi cha kwanza kutokana na kushindwa kuonyesha makeke aliyokuwa nayo awali.

Aliibukia ndani ya Aston Villa akitokea Klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji na ni mtazania wa kwanza kucheza Ligi Kuu England ambayo ni namba moja kwa kufuatiliwa duniani.

Akiwa ndani ya Villa, Samatta aliweza kutupia mabao mawili na timu yake ilikuwa kwenye hatihati ya kushuka daraja ila iliponea kwenye tundu la sindano baada ya kushinda mchezo wake wa mwisho.

Leave A Reply