Samatta Arejea Ubelgiji, Royal Antwerp
Mshambuliaji wa Kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta amesajiliwa kwa mkopo wa msimu mzima na Klabu ya Ubelgiji, Royal Antwerp FC akitokea Klabu ya Uturuki, Fenerbahce
Samatta amewahi kucheza katika Ligi Kuu ya Ubelgiji akiwa na Klabu ya KRC Genk na kuisaidia kuwa Bingwa miaka miwili iliyopita kisha kuhamia Aston Villa na kisha kwenda Fenerbahçe