The House of Favourite Newspapers

Samatta Atembelea Coca-Cola Tanzania, Azindua Kampeni Ya Washa Mdundo

0
Meneja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola Tanzania, Kabula Nshimo (kushoto), akimuonyesha nahodha wa timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ na mshambuliaji wa Klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki, Mbwana Samatta hatua za utengenezaji wa kinywaji cha Coca-Cola wakati alipotembelea kiwandani hapo. Samatta ambaye pia ni mwakilishi wa Coca-Cola Tanzania wa kuitangaza chapa ya kampuni hiyo katika kampeni zake ili kuwahamasisha Watanzania kufikia ndoto zao, alishirika kwenye uzinduzi wa kampeni ya ‘WASHA MDUNDO.’
Nahodha wa timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ na mshambuliaji wa Klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki, Mbwana Samatta (Kulia), akipata maelekezo kutoka kwa Meneja wa Kitecho cha Ufungaji cha Coca-Cola Kwanza, Jamah Adam (Kushoto) kuhusu mchakato mzima wa utengenezaji wa kinywaji cha Coca-Cola.
Menenja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola Tanzania, Kabula Nshimo (kushoto), akimkabidhi zawadi nahodha wa timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ na mshambuliaji wa Klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki, Mbwana Samatta wakati alipotembelea kiwanda cha kampuni hiyo.
Mbwana Samatta (Katikati), akipata maelekezo kutoka kwa Mkurugenzi wa Mauzo wa Coca-Cola Kwanza, Eric Ongara (Kulia) kuhusu kinywaji cha Coca-Cola na shughuli zake nchini wakati alipotembelea kiwandani hapo. Kulia ni Mkurugenzi wa Uchukuzi wa Coca-Cola Kwanza, Haji Ally Samatta ambaye pia ni mwakilishi wa Coca-Cola Tanzania wa kuitangaza chapa ya kampuni hiyo katika kampeni zake ili kuwahamasisha Watanzania kufikia ndoto zao.
 Mbwana Samatta (Kushoto), akijibu maswali ya waandishi wa Habari (hawapo pichani) wakati alipotembelea kiwanda cha kampuni hiyo kujionea mchakato mzima wa utengenezaji wa kinywaji cha Coca-Cola. Pamoja naye kushoto ni Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Samatta, Habuna Habibu Makanyangiro.
DJ D Ommy au maarufu kama ‘The International DJ’ naye alikuwepo kwenye uzinduzi wa kampeni ya ‘WASHA MDUNDO’ ya kampuni ya Coca-Cola Tanzania.
Menenja Mwandamizi wa Chapa ya Coca-Cola Tanzania, Kabula Nshimo (kushoto), akiwa amepozi katika picha na Mbwana Samatta.

Nahodha wa timu ya Taifa, ‘Taifa Stars’ na mshambuliaji wa Klabu ya Fenerbahce ya Ligi Kuu ya Uturuki, Mbwana Samatta leo Juni 1, 2021 ametembelea Kiwanda cha Cocacola kujionea hatua za utengenezaji wa kinywaji hicho. Samatta ambaye pia ni mwakilishi wa Coca-Cola Tanzania wa kuitangaza chapa ya kampuni hiyo katika kampeni zake ili kuwahamasisha Watanzania kufikia ndoto zao, alishirika kwenye uzinduzi wa kampeni ya ‘WASHA MDUNDO.’

Leave A Reply