The House of Favourite Newspapers

Samatta, Ulimwengu wasaka rekodi Afrika

0

SamataBwana580211.jpgMbwana Samatta .

LEO Jumamosi kwenye Uwanja wa TP Mazembe jijini hapa, kikosi cha TP Mazembe kitacheza mechi ya marudiano ya fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya USM Alger ya Algeria.
Katika mchezo wa awali kwenye Uwanja wa Omar Hamadi jijini Algiers, Algeria, Mazembe ilishinda mabao 2-1, hivyo wenyeji sasa wanahitaji sare tu kutwaa ubingwa.
Kwenye kikosi cha Mazembe, wamo Watanzania Mbwana Samatta na Thomas Ulimwengu ambao wanaweza kuandika historia ya kutwaa ubingwa huo wa Afrika endapo timu yao itabeba taji hilo.
Ukiachana na rekodi hiyo, Samatta ambaye ni straika wa zamani wa Simba, pia anawania kutwaa tuzo ya ufungaji bora kwani ana mabao saba sawa na Bakri Al-Madina wa El Merreikh ya Sudan ambayo imetolewa awali.
Hii ni nafasi ya kipekee kwa Samatta kwani kama akifunga hata bao moja atakuwa ametwaa Tuzo ya Ufungaji Bora Afrika na kuweka rekodi ya kuwa Mtanzania wa kwanza kufanya hivyo.
Baada ya mchezo huo, Samatta na Ulimwengu watajiunga na kambi ya Taifa Stars huko Afrika Kusini kujiandaa na mchezo wa kufuzu Kombe la Dunia 2018 dhidi ya Algeria.

Leave A Reply