The House of Favourite Newspapers

Sarah: Harmonize ameishikilia roho yangu

WENGINE roho zao zikiwa zimeshikiliwa na Mwenyezi Mungu, kwa upande wa mke wa mwanamuziki Rajabu Abdul ‘Harmonize’ Sarah roho yake imeshikiliwa na mumewe huyo.   Sarah aliiambia Za Motomoto ya Risasi kuwa kutoka moyoni mwake kila tone la penzi lake la kweli lipo kwa mumewe huyo kiasi ambacho anaamini kabisa moyo wake kaushika na si mtu mwingine.

“Kwa kweli nimependa na nimemaanisha kweli, maana kuna wakati najiona kabisa kama moyo wangu kaushikilia yeye mkononi akiudosha basi lakini penzi langu la kweli lipo kwa mumewe wangu kumchoka itakuwa kazi sana,” alisema Sarah.

Stori: IMELDA MTEMA

Comments are closed.