The House of Favourite Newspapers

Sasha: Naolewa Kutoa Nuksi

0
Sasha Kassim.

MWANADADA mwenye mvuto wa aina yake Bongo, Sasha Kassim ambaye anatarajia kufunga ndoa mwanzoni mwa mwaka kesho amesema kuwa, ameamua kuolewa ili kutoa nuksi.

 

Sasha ambaye hujulikana sana mitandaoni kwa picha zake za kihasara, alisema hadi sasa bado hajaenda kutambulishwa ukweni na wala hakuna mpango huo, ila amekuwa akiwasiliana na wakwe zake kwa njia ya simu, baada ya ndoa ndipo ataenda kupata baraka zao lakini makazi yake yataendelea kuwa Bongo.

 

“Naolewa kutoa nuksi si unajua mwanamke kukaa bila ndoa haileti picha nzuri, wakwe zangu wamenikubali japo hawajawahi kuniona laivu zaidi ya kwenye simu, nimeshaongea na mume wangu mtarajiwa kwamba akinioa nitaendelea kuishi Bongo, sababu napapenda sana huko Italy nitakuwa naenda kwa muda mfupi na kurudi na amekubali,” alisema Sasha ambaye anatarajia kuolewa na Bonphace, raia wa Italy.

Stori: Mayasa Mariwata.

Matukio kama haya na mengine, Install App Yako ya Kijanja na Namba Moja Tanzania ya Global Publishers

Android ===>Google Play

iOS ===>Apple Store

VIDEO: DK SHIKA KUWEKA HISTORIA USIKU WA 900 ITAPENDEZA

Leave A Reply