The House of Favourite Newspapers
gunners X

SBL kuendelea kuchangia maendeleo ya kilimo nchini kupitia elimu

0
MkurugenziMtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Mark Ocitti (aliyevaa kofia) akiongea na waandishi wa habari muda mfupi baada ya kumalizika kwa ziara ya wanafunzi wa Chuo cha Kilimo cha Mt. Maria Goretti ambao ni wanufaika wa Programu ya ufadhili wa masomo wa kampuni hiyo unaojulikana kama Kilimo Viwanda katika shamba la Silverlands lililopo Ifunda mkoani Iringa. Kulia aliyevaa miwani ni mmoja wa wafanyakazi wa shamba hilo Janet Senders

Kampuni ya Bia ya Serengeti Breweries Limited (SBL) imedhamiria kuendelea kutengeneza maisha bora kwa vijana na wakulima nchini kupitia programu yake ya udhamini wa masomo kwa wanafunzi wanaotoka familia masikini kwenye vyuo vinavyofundisha kilimo.

Programu hii iliyoanzishwa mwaka 2010 imesaidia wanafunzi 71 kusomea kozi za diploma katika ujuzi wa kilimo katika vyuo vinne kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa SBL, Mark Ocitti.

Katika tukio la kuwapongeza wanafunzi 17 waliopata nafasi za ufadhili kupitia programu hii kutoka chuo cha Mt Maria Goretti Agriculture Training Institute, Ocitti alinukuliwa akisema kuwa Kilimo Viwanda imelenga kusaidia wanafunzi kutoka familia masikini ili waweze kusomea masomo ya kilimo kwenye ngazi ya diploma katika vyuo vya ndani.

Meneja wa shamba la WayneTraves (aliyechuchumaa)akiwaelekeza jambo kuhusu udongo wanafunzi wa Chuo cha Kilimo cha Mt. Maria Goretti Pamoja na wafanyakazi wa SBL ikiwamo MkurugenziMtendaji Mark Ocitti (aliyevaakofia)walipotembelea shamba hilo.

Wanafunzi wengine 43 chini ya programu hii wanapatikana Kaole Wazazi College of Agriculture (Bagamoyo), Kilacha Agriculture and Livestock Training Institute (Moshi) na Igabiro Training Insitute of Agriculture (Bukoba).

Ocitti alifafanua kuwa ufadhili huu unajumuisha malipo yote ya chuo na gharama zingine katika kipindi chao chote cha masomo. Vilevile, Kilimo Viwanda inalenga kuongeza nguvu

jitihada za Serikali katika kuimarisha sekta ya kilimo kwa kuongeza idadi ya wataalamu wa mashamba watakaowasaidia wakulima kuboresha mashamba yao. SBL inategemea kwa kiasi kikubwa mazao ya nafaka kama vile mtama, shayiri na mahindi katika uzalishaji wao.

Vile vile Ocitti alisema, ‘Programu hii ni fursa nzuri kwa wanafunzi kuongeza upeo wao kwa kujifunza kimatendo watakapotembelea mashamba makubwa ya wakulima wanaolima nafaka kama hizi pamoja na kutembelea viwanda vyetu vya Dar es Salaam, Moshi na Mwanza ili kushuhudia namna kilimo na uzalishaji unavyotegemeana.’

Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Mark Ocitti (aliyevaa kofia) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa Chuo cha Kilimo cha Mt. Maria Goretti ambao ni wanufaika wa Programu ya ufadhili wa masomo wa kampuni hiyo unaojulikana kama Kilimo Viwanda katika muda mfupi baada ya kumalizika kwa ziara katika shamba la Silverlands lililopo Ifunda mkoani Iringa. Wengine kwenye picha ni wafanyakazi wa shamba hilo na wafanyakazi wa SBL

Mkuu wa Chuo hicho, Isaya Marcus Kigava hakuwa nyuma kusema, ‘naipongeza na kuishukuru sana kampuni ya Serengeti kwa kusudi lao zuri la kuwasaidia wanafunzi hawa katika kuboresha maisha yao ya baadae. Ni programu muhimu sana kuwapa elimu ya kimatendo ili waweze kufanya vyema kwenye kilimo cha biashara. Daima tutaukumbuka mchango wenu’

SBL inatoa ufadhili wa masomo kwa wanafunzi kutoka vyuo vinne kwenye programu hii ya Kilimo Viwanda ambavyo ni; Kaole Wazazi College of Agriculture (Bagamoyo) ambapo wanafunzi 15 tayari washatangazwa; Kilacha Agriculture and Livestock Training Institute (Moshi), na Igabiro Training Insitute of Agriculture (Bukoba) watakaotangazwa siku za usoni.

Stori: Na Mwandishi Wetu

Leave A Reply