Sekeseke la Mastaa na Unga ni Fundisho
NA ANDREW CARLOS |IJUMAA | SHOW-BIZ
ZIKIWA zimepita siku mbili tangu Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ya jijini Dar es Salaam kuwaachia kwa dhamana wasanii 13 kwa tuhuma za kutumia madawa ya kulevya, baada ya kuhenya chini ya uangalizi wa Jeshi la Polisi, sekeseke hilo ni vyema likachukuliwa kama fundisho kwao na wengine ambao hawajatajwa.
ILIKUWAJE?
Mwanzoni mwa mwezi huu, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda aliwataja wasaniii wanaotuhumiwa kwa matumizi ya dawa hizo huku mastaa wengi wa Bongo Fleva na filamu waki w e m o kwenye l i s t i hiyo.
Miongoni mwa wasanii hao ni Hamidu Chambuso (Dogo Hamidu au Nyandu Toz), Rajabu Salum (Mchafu Chakoma), Romeo Bangura (Rommy Jons), Cedou Madigo (Babuu wa Kitaa), Khalid Mohammed (T.I.D), Johana Mathysen (Director Johan), Winfrida Josephat (Recho Kizunguzungu) Anna Kimaro (Tunda), Wema Sepetu, Lulu Abbas (Lulu Diva) na Ahmed Hashim (Petit Man).
SEKESEKE KIVIPI?
Ukiachana na kutajwa na kutakiwa kufika katika Kituo Kikuu cha Polisi (Central), mastaa hao walitii amri hiyo lakini kitu kikubwa kwao ni sekeseke walilokutana nalo kuanzia siku ya kwanza walipotajwa na kukaa selo kwa zaidi ya siku tatu na wengine mbili.
Mastaa wengi walipotajwa majina yao na kutakiwa kufika kituoni hapo, walijua ni ishu ya kwenda kuhojiwa na kurudi lakini ikawa ndivyo sivyo kwani walijikuta wakiwekwa selo kwa siku hizo. Mbali na kuwekwa ndani huko, familia nyingi za wasanii hao zilikuwa njia panda baada ya ndugu na watoto wao kuhusishwa na matumizi hayo na pia kulazwa kituo cha polisi.
Tunda
Sekeseke lingine ni siku ya kufikishwa mahakamani ambapo mastaa waliotuhumiwa wakiongozwa na TID, Nyandu Toz, Rommy, Mchafu na Babuu walikuwa chini ya ulinzi wa Jeshi la Polisi kutokea central ambapo walipandishwa kwenye ‘difenda’ ya polisi na hata walipofikishwa nje ya mahakama walipangishwa foleni ya kuchuchumaa mmoja mmoja.
Walionekana kutokuwa na furaha, sura zao zilikuwa za huzuni na kuwafanya hata ndugu zao nao kuwaonea huruma. Ilikuwa ni fedheha kwao hasa ukichukulia ile hadhi waliyokuwa nayo huko mtaani kama mastaa lakini pia kile walichotuhumiwa nacho.
Recho
Yawezekana wapo wanaojutia kwa kuwa wanatuhumiwa kwa kitu ambacho kweli wanakifanya. Kama ni hivyo, basi kujuta huko kuwe sababu ya wao kubadilika.
Ukijaribu kufuatilia kwa karibu utagundua kuwa nia ya Mheshimiwa Makonda haikuwa mbaya, alifanya vile katika jitihada za kupambana na tatizo hilo ambalo limekuwa ni tisho katika jamii yetu.
TID
Lakini pia baadhi ya waliokuwa na msala huo waliwahi kutuhumiwa huko nyuma lakini walikuwa wakikana wakisema wanasingiziwa. Kwa hapa walipofikia ni vyema kwa kile kilichowapata kikawa ni fundisho kwao na wanachotakiwa kufanya ni kubadilika tu.
Inafahamika kwamba, kujihusisha kwa namna yoyote na mambo ya madawa ya kulevya ni kosa kisheria ambalo linaweza kukuharibia maisha yako, sasa kama wewe ni msanii mwenye future yako, kwa nini ujiingize huko? Hujitaki?
Rommy Jons
Labda niseme tu kwamba, waliotuhumiwa kwenye soo hilo la unga wanatakiwa kuchukua hatua za haraka za ‘kuyapaka rangi’ majina yao badala ya kuendelea kuyachafua. Pia iwe fundisho kwa wengine ambao wanatumia, wanauza au kusafirisha lakini kwenye awamu hii hawakutajwa. Huenda siku wakitajwa wakahenyeka zaidi ya wenzao waliotangulia.
Petit Man
Hili lisiwe kwa mastaa tu, hata wengine wanaojihusisha na madawa ya kulevya ni vyema wakachukulia hiki kilichowapata mastaa hao kama fundisho kwao. Ni imani yangu kwamba, kwa joto ya jiwe walilopata mastaa hao itakuwa ni chachu ya mabadiliko kwa jamii nzima.
WALIPO MASTAA HAO
Kwa sasa baadhi ya mastaa hao wakiongozwa na TID na Tunda wapo nje kwa dhamana baada ya mahakama kutoa uamuzi wa kuwa chini ya uangalizi kwa kipindi cha mwaka mmoja kwa mujibu wa kifungu cha 73 (e) na 74 cha Mwenendo wa Makosa ya Jinai kilichofanyiwa marekebisho mwaka 2002 na kujidhamini wenyewe kwa dhamana ya Sh. Milioni 10 kila mmoja pamoja na kuripoti Central Polisi kwa mwezi mara mbili.
Comments are closed.