The House of Favourite Newspapers

SEPTOL; DAWA KIBOKO KWA KUUA VIJIDUDU VYA MARADHI

Mazingira tunayoishi yamejawa na vitu vingi vinavyoweza kusababisha maambukizi ya vijidudu vya magonjwa mbalimbali, kama bakteria, fangasi, virusi na kadhalika ambayo huathiri afya ya binadamu.

 

Kuanzia asubuhi unapoamka, unapitia kwenye mazingira mengi yanayohatarisha afya yako, unashikana mikono na watu, unashika vitu vichafu na wakati mwingine unapata michubuko na majeraha yanayoweza kusababisha ukapatwa na maambukizi ya bakteria mwilini.

 

Ni kwa sababu hii ndiyo maana Kampuni ya Emina Medics Company Limited ikazindua dawa bora na ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kupambana na vijidudu vya maradhi, iitwayo Septol.

“Dawa hii iliyopo katika mfumo wa majimaji, inao uwezo mkubwa wa kupambana na aina nyingi za vijidudu vya maradhi, bakteria, fangasi na virusi ndani ya muda mfupi na unaweza kuitumia kwa urahisi kabisa kwa matumizi mbalimbali yatakayoondoa vijidudu vyote vya maradhi kwenye mwili wako na kwenye mazingira yanayokuzunguka,” anasema Zahara Mohamed, mwakilishi wa kampuni hiyo.

 

Zahara anaongeza kwamba: “Ukitoka kwenye shughuli zako za kutwa nzima, kabla ya kufanya chochote, unashauriwa kunawa mikono yako kwa Septol, kisha baada ya hapo, maji utakayoenda kuoga pia unayachanganya na dawa hii kwa kiasi cha mililita 15, hapo utakuwa na uhakika wa asilimia 100 kwamba mwili wako uko safi kabisa.”

 

Kama nguo zako pia unahisi zinaweza kuwa na bakteria na vijidudu vya maradhi, unashauriwa kuchanganya dawa hii kwenye maji unayofulia kwa kiasi cha mililita 25, nguo zako zitakuwa safi na salama.

Katika mazingira ya nyumbani, Septol pia inaweza kutumika kusafishia vyoo, mabafu, masinki, sakafu na maeneo mengine yenye uchafu hatarishi ambapo uwezo wake wa ajabu, utaondoa vimelea vyote vya maradhi na kuyafanya mazingira uliyopo, yawe safi na salama.

 

Mbali na matumizi hayo lukuki, pia Septol inaweza kutumiwa kwa usafi wa akina mama waliotoka kujifungua, kwa usafi wa mahospitalini, saluni na kwenye maeneo yote yenye hatari ya kuwepo vimelea vya magonjwa na kukufanya uwe salama kwa asilimia 100. Pia dawa hii inaweza kutumika kusafishia majeraha ya kujikata, magonjwa ya ngozi na vidonda visivyopona.

 

“Bidhaa zetu zinapatikana nchi nzima na tunaweza kukuletea mahali ulipo kama unahitaji oda kubwa, unachotakiwa kufanya ni kuwasiliana na wauzaji wetu waliopo jirani na wewe. Kwa jijini dar es Salaam, ofisi zetu zipo Upaanga jijini Dar es Salaam na unaweza kuwasiliana nasi kwa namba 0745 215 253 au 0688 618 139.

“Kwa wale waliopo mikoani, wanaweza kuwasiliana na wauzaji wetu kama ifuatavyo: Mwanza, Mara, Geita na Shinyanga, piga simu namna 0763699918, kwa Arusha, Manyara na Simiyu, piga namba 0764559026.

 

“Kwa wateja waliopo Kilimanjaro, Tanga na Kigoma, wawasiliane na wauzaji wetu kwa namba 0784744410, wale wa Njombe wapige namba 0759185344, Lindi na Mtwara namba 0757409134, Dodoma, Singida na Tabora namba ni 0716664444 na kwa wale wa Bukoba, Katavi na Rukwa, wapige namba 0752104085,” alisema Zahara.

 

Tazama video hii ujifunze zaidi

Comments are closed.