The House of Favourite Newspapers

Serikali Ya China Yapongezwa Kukuza Somo la Lugha ya Kichina Hapa Nchini

0

Katibu Mkuu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Profesa Carolyne Nombo ameishukuru Serikali ya China kwa juhudi inazoonesha katika kuhakikisha somo la lugha ya Kichina linafundishwa kwa ufasaha nchini.

Profesa Nombo ametoa shukrani hizo jijini Dar es Salaam wakati akipokea msaada wa vitabu 2,700 kutoka nchini China kwa lengo la kuwezesha ufundishaji na ujifunzaji wa lugha ya kichina.

Amesema ufundishaji wa lugha ya kichina kwa wanafunzi wa kidato cha kwanza hadi cha nne hapa nchini umeendelea kuimarika tangu kuanzizshwa kwake mwaka 2016.

“Kwa sasa ziko shule za Serikali 18 zinazofundisha lugha ya kichina, Shule mbili ambayo ni Morogoro na Usagara zimechukua hatua zaidi na kufundisha lugha hiyo kwa wanafunzi wa kidato cha tano wanaochukua mchepuo wa Kiswahili, kingereza na lugha ya kichina (KEC),”amesema Profesa Nombo.

Profesa Nombo ameongeza kwa sasa wizara ipo kwenye mapitio ya Sera na mabadiliko ya mitaala na moja ya mapendekezo yaliyopo ni kufundisha lugha mbalimbali ambapo wachina wameanza.

“Nimeelezwa kuwa mwezi Aprili 2023 mligawa vitabu 2,304 na leo vitabu 2,700 na kufanya idadi ya vitabu mlivyotoa kuwa 5004 hii itasidia katika ufundishaji na ujifunzaji wa lugha ya kichina na kuleta uwiano mzuri wa vitabu kwa wanafunzi ,”amesema Profesa Nombo

Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania CHEN Mingjian amesema urafiki wa Tanzania na China ni wa muda mrefu na kwamba wanaendelea kuufurahia.

Amesema anaamini siku zote maarifa yana nguvu, hivyo vitabu vilivyogawiwa vitasaidia walimu na wanafunzi kujifunza lugha ya Kichina kwa ufasaha ikiwa ni pamoja na kuielewa historia ya nchi ya China na utamaduni wao.
Kwa mara nyingine Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imekutana na Wadau wa Maendeleo jijini Dar es Salaam kuwapitisha, kujadili na kupokea maoni juu ya Rasimu ya Sera na mafunzo ya Mwaka 2014 toleo la 2023 na Rasimu ya Mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Ualimu.

Akizungumza katika kikao kazi hicho, Waziri wa Elimu Mhe. Prof. Adolf Mkenda amesema Wizara itaendelea kushirikiana na wadau hao katika kuhakikisha mageuzi ya elimu yanayofanyika yanafanikiwa.

“Mageuzi haya tunayofanya yanahitaji rasilimali katika kuyafanikisha, tuendelee kushirikiana ili yaweza kufanikiwa nasi tutaendelea kuwashirikisha katika kila hatuaā€¯,amesema Prof. Mkenda

Kwa upande wake Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Prof. Carolyne Nombo amewashukuru wadau hao kwa namna wanavyoendelea kufadhili miradi ya elimu yenye lengo la kuendelea kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia.

Mwenyekiti wa Wadau wa Maendeleo ya Elimu ambae pia ni Mkuu wa Sekta ya Elimu UNESCO Faith Shayo ameipongeza Serikali kwa mageuzi makubwa yanayofanyika kwenye elimu huku akiishukuru Wizara kwa kuwashirikia katika hatua mbalimbali kuelekea mageuzi hayo.

Leave A Reply