Serikali yalitaka Dira ya Mtanzania kukanusha tuhuma dhidi ya Balozi Ombeni Sefue
Mkurugenzi wa Idara ya Habari (MAELEZO) Bw. Assah Mwambene (katikati) akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es Salaam kuhusu taarifa za upotoshaji zilizotolewa na Gazeti la Dira ya Mtanzania la tarehe 29/02/2016 kuhusu Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Sefue, kulia ni Mkurugenzi Msaidizi Uratibu wa Vyombo Habari, Bw. Jamal Zuberi na Mkurugenzi Msaidizi Habari Bw. Vicent Tiganya wote kutoka Idara ya Habari (MAELEZO).
Baadhi ya waandishi wa habari wakifuatilia taarifa iliyokuwa ikitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Habari, Bw. Assah Mwambane (ambaye hayupo katika picha) iliyokuwa ikiutaka uongozi wa Gazeti ya Dira Mtanzania kukanusha habari waliyoitoa hivi karibuni iliyokuwa na kichwa cha habari “Uchafu wa Ombeni Sefue Ikulu”.