SERIKALI imetoa tamko rasmi likiyataka magazeti na majarida yote hapa nchini kusajiliwa upya kuanzia leo Alhamisi, Agosti 23 hadi hadi Oktoba 15, 2017 kwa mujibu wa sheria.
Msemaji wa Serikali Dk Hassan Abbasi ameyaeleza hayo leo wakati akizungumza na wanahabari katika Ukumbi wa Habari Maelezo, Posta jijini Dar es Salaam.
“Baada ya Oktoba 15, 2017 hakuna atakayeruhusiwa kuchapisha bila usajili”Amesema Dk Abbasi na kuongeza. Mfumo mpya wa utoaji wa leseni kwa machapisho yote umeanza rasmi leo ‘’
Amesema taratibu zote za upatikanaji wa leseni zimewekwa katika tovuti http://www.maelezo.go.tz “
Mawasiliano kwa ajili ya ufafanuzi kuhusu utaratibu wa usajili ni 0622664606 na 0717312417 au kupitia [email protected]
TAARIFA YA SERIKALI KWA UMMA
Global Publishers and General Enterprises Limited is a registered private company dealing in publishing of weekly Swahili newspapers in Tanzania, namely; Uwazi, Ijumaa, Championi, Amani, Risasi & Ijumaa Wikienda.
Prev Post