The House of Favourite Newspapers

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 34

0

ILIPOISHIA:

Safari hii maneno hayakuwa mengi, tuliendelea kupasha miili yetu, tayari kwa ngwe ya pili ya pambano letu la kirafiki. Safari hii yeye ndiye aliyekuwa akiniongoza nini cha kufanya, nami nikawanafuatisha kwa utii mkubwa, haikuchukua muda, kipyenga kikalia kuashiria kuanza kwa ngwe ya pili, huku safari hii akionesha kupania kuwa nyota wa mchezo.

SASA ENDELEA…

Mikikimikiki iliendelea, kwa mud nilisahau kama nilikuwa mgonjwa ambaye haukuwa umepita muda mrefu tangu nizinduke kutoka kwenye usingizi wa kifo, wala usingeweza kuamini kwamba ndiye mimi ambaye nilifikishwa hospitalini kila mmoja akiamini kwamba siwezi kurejewa na fahamu zangu.

“Jamal! Jamaa..aa..al!” Shamila alipiga ukelele na kunikumbatia kwa nguvu kifuani kwangu kuonesha kwamba tayari alishasalimu amri, mapigo ya moyo wake yakawa yanamuenda mbio kuliko kawaida, huku kila kiungo cha mwili wake kikiwa kimelegea kama mlenda.

Akaangukia pembeni, na mimi nikaangukia upande mwingine, huku kijasho chembamba kikinitoka. Ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kuna majimaji yalikuwa yakinitoka pale kwenye jeraha langu, nikahisi huenda ni jasho.

Nilipopeleka mkono na kujishika kisha nikausogeza mkono machoni, nilishtuka kupita kiasi baada ya kugundua kuwa zilikuwa ni damu znanitoka pale kwenye jeraha langu.

“M ungu wangu,” nilisema huku nikiinuka harakaharaka na kusogea kwenye kioo cha dressing table ya kisasa iliyokuwa ndani ya chumba hicho cha Shamila. Bandeji yote ilikuwa imelowa kwa damu kuashiria kwamba kumbe zilikuwa zimeanza kunitoka muda mrefu uliopita.

Kumbe zile purukushani na Shamila zilikuwa zimenitonesha lakini cha ajabu, wala sikusikia maumivu yoyote mpaka muda huo. Nadhani utamu wa pambano letu la kirafiki ulifanya kazi kama sindano ya ganzi, kweli waliosema mapenzi yana nguvu ya ajabu hawakukosea.

>>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

Cha ajabu, eti tayari Shamila alikuwa akikoroma kwa uchovu, ikabidi nimtingishe kwa nguvu huku nikiliita jina lake. Alionekana kuwa mzito sana, akafumbua macho kivivu na kunitazama.

“Amka, angalia mwenzio kilichonitokea,” nilimwambia huku nikimuonesha kifua change, nikamuona jinsi alivyoshtuka, japokuwa mwili wake haukuwa na nguvu, alkijikongoja na kuamka, akawa anashangaa nini kimetokea.

Harakaharaka alichukua upande mmoja wa khanga na kujifunga akainuka na kunisogelea, akionesha kuwa na hofu kubwa ndani ya moyo wake.

“Pole Jamal, ooh! Mimi ndiyo nimekusababishia,” alisema na kunibusu, harakaharaka akatoka huku akikimbia, macho yangu yakawa yanamsindikiza kwa nyuma, japokuwa nilikuwa kwenye hali mbaya, nilijikuta nikitabasamu kwani kilichotokea ilikuwa sawa na nzi kufia kwenye kidonda, umbile lake likaacha mtikisiko adhimu na kunifanya nitingishe kichwa changu.

Muda mfupi baadaye, alirejea akiwa na kiboksi kidogo cha huduma ya kwanza kilichokuwa na alama ya msalaba mwekundu, akanilaza kitandani na kuanza kunihudumia. Cha ajabu zaidi, safari hii wala sikuhisi kabisa maumivu, nikawa muda wote namtazama Shamila usoni.

Waliosema mapenzi hayajaribiwi hawakukosea, japokuwa mwenyewe nilikuwa najiona kama namzuga Shamila, kwa yale ‘maujanja’ aliyonionesha, nilijikuta akianza kuugusa moyo taratibu, nikawa naendelea kumtazama wakati mwenyewe akinihudumia kwa unyenyekevu wa hali ya juu.

“Mbona unaniangalia usoni, mi nasikia aibu bwana,” alisema huku akinitazama kwa macho yake yaliyoonesha dhahiri jinsi alivyokuwa amechoka, wote tukatabasamu.

“Haya inuka nimalizie kukufunga bandeji,” alisema, ni hapo ndipo nilipogundua kwamba kumbe tayari alishamaliza kunifungua ile bandeji iliyokuwa imelowa damu na kunifunga nyingine, nikainuka kwa umakini kwani hii ilikuwa mara ya pili kujitonesha, akamalizia kunifunga, akarudia kunipa pole na kunibusu kwenye paji la uso wangu.

Akaanza kubadilisha lile shuka pale kitandani kwake ambalo nilikuwa nimelichafua, huku akiendelea kuniomba radhi kwa kunitonesha, nikawa nachekacheka tu.

>>> Usikose kutembelea Simulizi za Majonzi

“Muda umeenda sana, watakuwa wanakutafuta hospitali, inabidi nikurudishe haraka,” alisema, nikaangalia saa ya ukutani na kugundua kuwa tulikuwa tumetumia muda mrefu sana nje ya hospitali, kinyume na utaratibu kwani ikumbukwe kwamba nilikuwa nimelazwa wodini ila njama zangu na Shamila ndiyo zilizowezesha mimi kutoka.

“Naomba unisaidie kitu kimoja,” nilimwambia Shamila wakati akiandaa mazingira ya sisi kwenda kuoga, baada ya kuwa nimeshakunywa dawa za kutuliza maumivu alizonipa baada ya kumaliza kunifunga jeraha langu.

“Jambo gani mpenzi wangu wa moyo,” alisema Shamila huku akiniegamia kwa kudeka, nikamwambia naomba aniazime simu yake nihamishe baadhi ya mafaili kutoka kwenye kompyuta ili nikaendelee kuyapitia nikiwa wodini.

“Kwani ni mafaili gani? Halafu kwa nini uyakopi kwenye simu wakati nina laptop?” alisema, jambo lililonifurahisha sana kwani alikuwa amenirahisishia sana kazi, nikamzugazuga pale, akatoka na kwenda kwenye chumba cha pili, aliporudi alikuwa na laptop ndogo mkononi, akanipa huku tabasamu pana likiwa limechanua kwenye uso wake.

Nilimshukuru sana, harakaharaka nikaenda pale sebuleni, nikaiunganisha laptop na ile kompyuita ya mezani na kuanza kukopi mafaili yote yaliyokuwa kwenye ile hard disk niliyopewa na Firyaal, mdogo wake Shenaiza. Wakati mafaili yakiendelea kukopi, nilirudi chumbani kwa Shamila ambaye alikuwa amejilaza akinisubiri.

“Ahsante kwa yote uliyonifanyia Jamal, unajua mwanzo nilikuwa siamini kama kweli unanipenda, nilihisi kama mimi ndiyo nakulazimisha lakini kwa haya uliyonifanyia leo, hata sijui nikwambie nini, kwa kifupi elewa kwamba nakupenda sana na haijawahi kutokea mimi nikampenda mtu kama ilivyotokea kwako,” alisema Shamila kwa sauti yenye uwezo wa kumtoa nyoka pangoni, nikawa nachekacheka tu.

Aliinuka pale kitandani kichovu, tukaelekea bafuni ambapo aliniogesha kama mtoto mdogo huku akiwa makini maji yasiguse kidonda changu, alipomaliza, na yeye alioga kisha tukarudi chumbani ambapo harakaharaka tulivaa, tukatoka sebuleni ambapo nilienda kuchungulia pale kwenye kompyuta, nikakuta haijafika hata nusu kukopi.

“Inabidi nikukaangie mayai ule harakaharaka tuondoke,” alisema Shamila huku akimalizia kuvaa vizuri nguo zake za kazini, nikakosa cha kumjibu kwa sababu kiukweli nilihitaji muda zaidi ili nikopi yale mafaili yote.

Aliwasha jiko la gesi, akanikaangia mayai na dakika tatu tu baadaye, tayari yalikuwa tayari, akaniandalia mezani na juisi, nikaanza kula taratibu ili angalau nivutevute muda, akampigia simu dereva teksi na kumuelekeza atufuate.

Cha ajabu, wala hakuonesha kutaka kujua nilikuwa nikihangaika na nini kwenye kompyuta, akaendelea kujiandaa kwa kujipodoa kama ilivyo kawaida ya wanawake muda mfupi baadaye honi za gari zikasikika nje kuonesha kuwa tayari ile teksi aliyoiita ilishafika. Bado kompyuta haikuwa imefikisha hata asilimia ishirini na tano za kukopi, nikawa sina ujanja zaidi ya ‘ku-cancel’ palepale ilipoishia, nikiamini lazima kuna mambo mengi tu yalishaingia kwenye ile laptop.

“Wala usiwe na wasiwasi, hapa ni kama kwako, kama hujamaliza kazi zako nitakuandalia utaratibu mwingine tuje tena,” alisema Shamila, nikakualiana naye. Nikaichomoa ile laptop na kuzima kompyuta huku ile hard disc ikia ndani yake. Nilijua nafanya makosa lakini nikaamini Shamila hawezi kuiwasha hiyo kompyuta kwa sababu kwanza hakuwa akiijua password.

Harakaharaka tukatoka na kuingia ndani ya teksi, safari ya kurudi hospitalini ikaanza huku muda wote Shamila akiwa na furaha ya ajabu, akawa ananimwagia mvua ya mabusu.

Dakika kadhaa baadaye, tuliwasili hospitalini lakini mazingira ya pale yalinishtua mno, hofu kubwa ikaukumba moyo wangu tulipofika kwenye maegesho ya magari.

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue au bofya Simulizi za Majonzi.

Leave A Reply