The House of Favourite Newspapers

Seven Days in Hell (Siku Saba Kuzimu)- 52

ILIPOISHIA:

“Chukua taulo pale kabatini ingia bafuni ukaoge,” alisema akiwa amekaa juu ya kitanda kikubwa cha kisasa akihangaika kufungua zipu ya gauni alilokuwa amevaa, nikaelekea pale kwenye kabati aliponielekeza, nikachukua taulo na kuanza kuelekea kwenye lile bafu la ndani kwa ndani kule chumbani kwake.

Nililazimika kuingia na nguo zote bafuni kwani nilikuwa naona aibu kuvua hata shati mbele ya macho yake.

SASA ENDELEA…

“Sasa utaingiaje bafuni na nguo? Hebu toa ushamba wako hapa,” alisema Junaitha huku akicheka, nikajikuta nikiwa kwenye wakati mgumu sana. Japokuwa nilikuwa nimeshaingia, ilibidi nitoke, nikajikaza kisabuni na kuvua fulana niliyokuwa nimeivaa, bandeji iliyofungwa juu ya jeraha langu ikaonekana vizuri.

“Mh! Kumbe uliumia kiasi hicho, hebu njoo nikuangalie,” alisema, nikavungavunga kwa aibu mwishowe nikasogea mpaka pale kitandani alipokuwa amekaa. Akanisogelea na kuanza kunitazama vizuri pale kifuani.

“Unajisikiaje kwani?” aliniuliza huku akiligusa jeraha langu kwa juujuu.

“Sasa hivi nina afadhali kubwa,” nilimjibu, akaendelea kulitazama jeraha hilo kwa muda kisha akaniambia nisiwe na wasiwasi, kuna dawa atanipaka ambayo itanifanya nipone haraka kuliko kawaida, niliitikia kwa kutingisha kichwa.

“Halafu mbona kama unaniogopa? Kwani nina tofauti gani na hao wanawake zako unaotoka nao? Au unaniona mimi mzee?” alisema huku mkono wake mmoja akiwa amenishika shingoni kwa upole. Kiukweli nilikuwa najisikia aibu sana kiasi kwamba sikuweza hata kumtazama usoni.

“Haya malizia kuvua nguo zako ukaoge na mimi nataka kuoga,” alisema huku akiniachia, nikashusha pumzi ndefu na kusogea pembeni ambapo niligeukia pembeni, nikalifunga lile taulo juu ya suruali kisha nikavua juu kwa juu, nikamsikia akiangua kicheko kutokana na ujanja nilioutumia.

“Mbona mimi sijishtukii kama wewe? Hebu niangalie,” alisema, nikageuka na kumtazama, nikamuona akilishusha gauni lake kwa maringo ya kikekike, macho yangu yakatua kwenye kifua chake, japokuwa alikuwa mtu mzima, alikuwa na kifua kama kigori. ‘Braa’ ya rangi ya zambarau iliyahifadhi vizuri maembe bolibo mawili yaliyokuwa yamejaa vizuri kama mtu ambaye hajawahi hata kuwa na mtoto.

Nikiwa bado nimepigwa na butwaa, nilimuona akimalizia kulitoa gauni lake lote, nilichokiona kilinifanya nipoteze ‘network’ kwa sekunde kadhaa, akaifungua na ile ‘braa’ aliyokuwa ameivaa, akabakia na nguo ya mwisho tu, mapigo ya moyo wangu yakawa yananienda mbio kuliko kawaida, nikameza funda la mate kama fisi aliyeona mfupa.

Japokuwa kwa nje alikuwa akionekana kama mtu mzima flani hivi, ndani Junaitha alikuwa tofauti kabisa, kwa makusudi kabisa akageuka kama anayetafuta kitu fulani, macho yangu yakatua kwenye mlima mkubwa uliokuwa upande wa nyuma, nikashusha pumzi ndefu huku kijasho chembamba kikianza kunitoka.

Ni kama alishaona kwamba ndege mjanja nimenasa kwenye tundu bovu kwani alisimama na kuanza kutembea kama wanamitindo wanavyotembea jukwaani, akanisogelea mpaka pale nilipokuwa nimesimama, akaipitisha mikono yake nyuma ya shingo yangu, tukagusanisha ndimi huku mikono yangu ikiwa bado haijui ishike wapi.

“Sitaki uniogope, mimi ndiyo mtu sahihi unayepaswa kuwa naye, nitakulinda na kukuepusha na matatizo yote unayoweza kuyapata kwa kubadili wanawake ovyo,” alisema kwa sauti ya kunong’ona, mdomo wake ukiwa sentimita chache kutoka kwenye sikio langu, sauti yake ikapenya hadi kwenye ngoma zangu na kuniongezea msisimko wa kipekee.

Nikajikuta mikono yangu imeenda kushikilia mlima wake, nikashtushwa na jinsi alivyokuwa na ngozi laini, nikamuona naye akishtuka kidogo kisha akaachia tabasamu pana, akaniachia shingoni na kunishika mkono, akawa ananivuta kama kondoo anayepelekwa machinjioni, nikawa namfuata, safari yetu ikaishia kwenye kitanda kikubwa cha kifahari.

Sikuelewa kilichoendelea mpaka nilipokuja kushtuka muda mfupi baadaye na kujikuta nikiwa kama nilivyokuja duniani, naye akiwa katika hali hiyohiyo, ‘Jamal’ wangu akiwa amechachamaa kupita kawaida. Kilichoendelea baada ya hapo, ilikuwa ni ‘experience’ nyingine mpya kabisa maishani mwangu.

Waliosema usidharau kitabu kwa kutazama kava lake hawakukosea, japokuwa kwa mwonekano Junaitha alikuwa akionekana mtu mzima flani hivi, alikuwa ‘fit’ mno, mpaka chombo kinatia nanga kwenye bahari ya huba kuashiria kufika mwisho wa safari, nilikuwa sijitambui, ukichanganya na ule uchovu wa kazi ya kumuokoa Shamila, nilijikuta nikipitiwa na usingizi mzito ambao nikiri kuwa sijawahi kuupata tangu nizaliwe.

Nilikuja kuzinduka baadaye na kujikuta nikiwa nimelala juu ya kitanda kilichotandikwa shuka jeupe na juu yake karatasi laini la nailoni, nikiwa nimefungwa taulo kubwa jeupe huku Junaitha naye akiwa amevaa nguo kama ya kulalia hivi, yenye rangi nyeupe.

Nilitaka kuinuka lakini akaniwahi na kunituliza, akaniambia ananisafisha kidonda changu na kunipaka dawa kama alivyoniambia, nikatulia. Nilimuona akichanganya dawa fulani kama mafuta hivi, akaja kuinyunyiza juu ya ile bandeji, muda mfupi baadaye akaitoa taratibu. Wala sikuhisi maumivu yoyote kama ilivyokuwa hospitali au wakati Shamila akinisaidia.

“Ungechelewa sana kupona kwa dawa za hospitali, inaonekana hili jeraha lilimaanishwa kuyakatisha maisha yako,” alisema huku akinimwagia dawa nyingine juu ya jeraha langu na kuanza kunichua taratibu, nikakosa cha kujibu zaidi ya kuwa namtazama tu usoni, kumbukumbu za yote yaliyotokea zikirudi kwa kasi kichwani mwangu.

“Nisamehe kwa kutangulia kukudharau, kumbe wewe siyo wa mchezomchezo,” alisema Junaitha, nikaachia tabasamu pana, aliendelea kunitibu lile jeraha na baada ya muda, aliniambia niinuke.

“Mbona hunifungi bandeji?” nilimuuliza huku nikijitazama pale kifuani.

“Wala hakuna haja, kitapona chenyewe, nakupa siku mbili tu lazima kiwe kimekauka ila inabidi upate muda wa kutosha wa kupumzika,” alisema, akaniongoza mpaka bafuni ambako kwa umakini mkubwa aliniogesha kama mtoto mdogo huku akizingatia maji yasiguse jeraha langu.

“Wameshaamka?”

“Ndiyo, ila ilibidi niwadanganye kwamba ulizidiwa tukiwa kule kwenye kazi kwa hiyo ndiyo nipo kukutibu, nakuomba sana uitunze hii siri, si unajua Shamila mimi ni mwanangu japokuwa sijamzaa mwenyewe, akijua itakuwa fedheha sana kwangu,” aliniambia, nikamtoa wasiwasi huku nikitaka kujua kwa nini tendo la mimi na yeye lilikuwa tofauti sana?

“Ni kama nguvu chanya na chanya zimekutana, hata mimi kuna mambo yamenitokea ambayo hayajawahi kunitokea tangu nipate akili zangu,” alisema Junaitha huku safari hii yeye ndiyo akiwa ananionea aibu, akishindwa hata kunitazama usoni mara mbili.

“Wewe ni mwanaume wa shoka,” alisema huku akinibusu kwenye paji la uso wangu, tukarudi chumbani ambapo nilivaa nguo zangu, akanishika mkono na kuniambia natakiwa ‘kuekti’ kama nasikia maumivu makali, akanitoa mpaka sebuleni ambako niliwakuta Shamila, Firyaal na Raya wakiwa wanatazama runinga kubwa ya ukutani.

Waliponiona tu, wote waliinuka haraka na kunikimbilia, kila mmoja akitaka awe wa kwanza kunifikia, nikamuona Junaitha akinitazama kwa macho yaliyoonesha kuwa na viulizo vingi, akawawahi:

“Bado hajapona, msimkumbatie kwa nguvu mtamtonesha!” Nikaona wote wameishiwa pozi, wakaishia kunishika mikono tu huku wakinitazama usoni, kila mmoja alionesha kuguswa mno na hali yangu, hakuna aliyekuwa anajua kwamba nilikuwa ‘nikiwaektia’, Junaitha ambaye pale ndiyo alikuwa mkubwa kuliko sisi wote, akawa ananitazama kama anayenisisitiza nisije nikaharibu.

Nikaenda kukaa kwenye sofa la peke yangu, wote wakanipa pole na nikawahakikishia kwamba nitakuwa sawa. Tukaanza kuulizana maana ya kile kilichofanyika mpaka tukafanikiwa kumuokoa Shamila ambapo Junaitha alianza kutufundisha mambo ambayo hakuna aliyekuwa akiyajua kati yetu, ambayo kama hujui ungeweza kusema ni uchawi wa hali ya juu.

“Hata ukitaka kuingia benki na kuchukua kiwango chochote cha fedha unachotaka, inawezekana, mbona rahisi tu, nitawafundisha,” alisema.

Je, nini kitafuatia? Usikose next issue. 

BREAKING DKT SLAA USO KWA USO NA MAGUFULI

Comments are closed.