The House of Favourite Newspapers

Shaa kumbe kama Beyonce tu

0

Shaa-672x372Shaa

Omary Mdose,
Dar es Salaam
MWANADADA Sarah Kaisi ‘Shaa’ anayefanya muziki wa Bongo Fleva, ameibuka na kusema haoni kitu cha ajabu kwake kuandikiwa wimbo kwani hata wasanii wa nje kama Beyonce huandikiwa pia.beyonce-grammy2015

BeyonceShaa anayetamba na Wimbo wa Toba alioutoa hivi karibuni, yupo mbioni kutoa wimbo mwingine ambao utakuwa umeandikiwa na Kundi la Yamoto Band.
“Wimbo wangu huu wa Toba umeandikwa na H-Mbizo, pia kuna mwingine unakuja umeandikwa na Yamoto Band, nimeamua kuandikiwa kwani nimeandika nyimbo nyingi na naona kama nikiendelea kufanya hivyo nahisi kama nitarudia kilekile.
“Sasa najaribu kubadili ladha, wasanii wengi hata wa nje ya Bongo wanaandikiwa kama kina Beyonce na wengine, kwani mimi nani mpaka isiwe hivyo?,” alihoji Shaa aliyekuwa memba wa Kundi la Wakilisha pamoja na Witness na marehemu Langa.

Leave A Reply