The House of Favourite Newspapers

Shabiki wa TP Mazembe Aitambia Simba: “Wasije na Paka” – Video

0

Mashabiki ambao walijitokeza Uwanja wa Mkapa walikuwa wachache kiasi chake na walishuhudia ushindani mkubwa ndani ya uwanja.

 

Kipindi cha pili wachezaji wa Al Hilal waliweza kukosa umakini dakika za mwanzo kupachika bao la pili huku TP Mazembe wenyewe pia wakikosa umakini kupachika bao la pili.

 

Ikiwa imebaki dakika moja mpira kukamilika, Al Hilal waliweza kupachika bao la pili dakika ya 89 kupitia kwa Mohamed Mussa ambaye alitumia makosa ya mabeki wa TP Mazembe kuokoa hatari iliyokuwa inakwenda langoni kwa kuzamisha mpira kambani.

 

Huu ni ushindi wa kwanza kwa Al Hilal ambapo mchezo wa kwanza walipoteza kwa kufungwa mabao 4-1 dhidi ya Simba.

 

Mashabiki wa Mazembe wametamba kuwa Simba hatatoboa katika Dimba la Mkapa lakini amewapa tahadhari kuwa wasiingie uwanjani na paka.

MSIKILIZE HAPA

Leave A Reply