Shamsa: Mastaa Wandeleze Wema wa Mwezi Mtukufu
BAADA ya hivi karibuni waumini wa dini ya Kiislamu kumaliza mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhani, msanii wa filamu Bongo, Shamsa Ford amewataka mastaa kuendeleza yale mema waliyokuwa wakifanya ndani ya mwezi huo na kuachana na kujiachia kihasara.
Akibonga na Za Motomoto News, Shamsa alisema ndani ya mwezi wa Ramadhani watu mbalimbali hasa mastaa walikuwa wakiuheshimu kwa kufanya yaliyo mema, kuvaa kiheshima na kutoachia video na picha za ajabu mitandaoni hivyo hata sasa waendelee hivyo hivyo ili kuendelea kumtukuza Mungu zaidi.
“Nawasihi mastaa waendeleze mema waliyokuwa wakiyafanya wakati wa Ramadhani, tusione wakiwa wanakaa nusu utupu au kufanya mambo mengine ya ajabu, wafanye ibada sana maana maisha yenyewe ni mafupi mno,” alisema Shamsa.
Comments are closed.