DAR ES SALAAM: KESI inayomkabili mtuhumiwa wa makosa ya kukamatwa na nyara za serikali, Yusuf Ali Yusuf maarufu kama Shehe Mpemba (35) ambaye alitajwa na Rais John Magufuli kuwa ndiye kinara wa biashara ya meno ya tembo, leo Januari 11, 2017 kesi hiyo imeahirishwa hadi Januari 24.
Akitaja kesi hiyo, Wakili wa Serikali katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Patrick Mwita mbele ya Hakimu Godfrey Mwambapa amewasilisha hoja kuwa upelelezi wa kesi hiyo umekamilika na jalada lipo kwa Zonal Criminal Officer (Z.C.O) analifanyia kazi ili aweze kulipeleka kwa Mwendesha Mashitaka wa Serikali (DPP).
HABARI: DENIS MTIMA/GPL
Comments are closed.