Shigongo Ampongeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa
Mbunge wa Buchosa, Eric Shigongo amempongeza Waruba Mwita, Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Buchosa kwa kazi nzuri aliyoifanya hususan katika ukusanyaji wa mapato.
Katika barua iliyoandikwa na Shigongo, huku nakala zikienda kwa Waziri wa Tamisemi na viongozi wengine, Shigongo amesema mapato ya mwezi ya halmashauri hiyo, yameongezeka na kufikia kiasi cha shilingi milioni 290 huku lengo likiwa ni kufikia shilingi milioni 400.