The House of Favourite Newspapers
gunners X

SHIGONGO AWAPA SIRI YA KUPATA ‘DIVISION ONE’ WANAFUNZI FORM 6

Shigongo akihamasisha nguvu ya ushindi kwa wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Saint Joseph ya jijini Dar es Salaam.

MKURUGENZI Mtendaji wa Global Group na Mwalimu wa Ujasiriamali, Eric Shigongo,  leo amezungumza na wanafunzi wa kidato cha sita wa Sekondari ya Saint Joseph iliyopo eneo la  Posta jijini Dar es Salaam na kuwapa mbinu za kufanya vizuri na kupata daraja la kwanza (division one) kwenye mtihani wao wa kuhitimu unaotarajiwa kuanza Mei 6 mwaka huu.

Wanafunzi wakisikiliza kwa makini.

Shigongo alikuwa katika shule hiyo kwa ajili ya kuzungumza nao na kuwapa hamasa kabla ya mitihani hiyo ambapo  aliwataka kujiandaa vyema katika mitihani hiyo ikiwa ni pamoja na kuondoa hofu na kujiamini kuwa wanaweza kukabiliana nayo.

Shigongo  akiwapa wanafunzi hao kitabu chake kinachohusu siri ya mafanikio maishani.

Mambo mengine aliyowafundisha pamoja na kujituma ni kuwa tayari kuumia kwa ajili ya maandalizi ya mitihani hiyo.

“Mnatakiwa kujituma sana hasa hiki kipindi kifupi kilichobaki, najua kwenye kujituma kuna changamoto nyingi.  Wakati mwingine unataka kujisomea na usingizi nao unajitokeza,  au uvivu unajitokeza, hivyo mnatakiwa kuishinda hali hiyo,” alisema.

Wanafunzi wakiwa na vitabu hivyo.

Jambo jingine muhimu alilowakumbusha katika kusaka ushindi wowote ni nidhamu.

Aliwataka pia kuweka nia ya kubadili historia za familia zao kwa kufanya mambo makubwa zaidi ya waliyofanya wazazi wao na kuwapa mfano kuwa iwapo baba aliishia digrii moja wao wapiganie kupata kuanzia digrii mbili.

Shigongo akiwa kwenye pozi la ucheshi na wanafunzi baada ya kumaliza kuongea nao akiwatakia mafanikio katika mitihani na maishani.

 

HABARI/PICHA: RICHARD BUKOS / GPL

Comments are closed.