The House of Favourite Newspapers

Shilole Afunga Ndoa na Uchebe Jijini Dar

Msanii Zuwena Mohamed ‘Shilole’ (katikati) akiwa na mpenzi wake waliyefunga naye ndoa, Ashraf Uchebe (kushoto) katika picha ya pamoja baada ya ndoa hiyo jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo.

Hatimaye msanii wa Bongo Fleva, Shilole amefungua ndoa na mpenzi wake Ashraf Uchebe huko Masaki usiku wa kuamkia leo jijini Dar es Salaam.

Staa huyo alikuwa akisisitiza kufunga ndoa mwaka huu lakini watu walikuwa wakichukulia poa kwa sababu si mara ya kwanza kutoa kauli kama hiyo lakini jana Desemba 6 akafanya kweli.

Ashraf Uchebe akiwa na mkewe, Shilole.

Baada ya picha kusambaa mtandaoni aliyekuwa mpenzi wa Shilole, Nuh Mziwanda ameandika ujumbe katika ukurasa wa Instagram ambao unaweza kutafsiriwa kama ametupa kijembe kwenye ndoa hiyo.  Nuh ameandika;

Alie LaLa na BiBi harusi’wiki Moja KabLa ya harusi’Na wala sio Bwana Harusi’Bado mnanishauri harusi 😏 (all girls are pretenders )

Alichokiandika Nuh Mziwanda ni mistari kutoka kwenye wimbo wa Mwana FA ‘Bado Nipo Nipo’ ambao ulitoka takribani miaka 10 iliyopita.

Comments are closed.