Sadick Muhidin (kushoto) akielekezwa na Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda (katikati) namna ya kujaza kuponi yake kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.
Wasomaji wa Gazeti la Uwazi eneo la Stendi ya daladala ya Vikindu wakijaza kuponi zao kushiriki droo ya Shinda Nyumba.
Mwanadada, Renatha Felix akiweka kuponi yake mara baada ya kumaliza zoezi la kuijaza.
Wadau wa Gazeti la Uwazi eneo la Vikindu-Mkuranga wakielekezana namna ya kujaza kuponi ili kuweza kushiriki zoezi la Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.
Zoezi likiendelea la kujaza kuponi kwa wakazi wa maeneo ya Vikindu-Mkuranga Pwani.
Ramadhani Mkalapema (katikati) akijaza kuponi yake ili kushiriki Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.Anayeshuhudia ni Ofisa Masoko wa Global,Yohana Mkanda.
Christina Michael (katikati) akielekezwa na Ofisa Masoko wa Global namna ya kujaza kuponi yake.
Wasomaji wa Maeneo ya Vikindu Mkuranga wakichangamkia kununua Gazeti la Uwazi ili kushiriki bahati nasibu hiyo.
Mwamvita Hemed akielekezwa na Ofisa Usambazaji wa Global, Jimmy Haroub (kushoto) ukurasa ulio na kuponi ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba.
Mwamvita akiweka kuponi yake mara baada ya kujaza kuponi kushiriki droo ya pili ya Shinda Nyumba.
Msomaji wa Gazeti la Uwazi akiweka kuponi yake kwenye ndoo maalumu ya bahati nasibu mara baada ya kuijaza.
Mmoja wa akina mama lishe akishiriki kuweka kuponi yake ya Shinda Nyumba.
Joel Paul (kushoto)akivalishwa kofia iliyo na nembo ya Shinda Nyumba msomaji wa Gazeti la Uwazi mara baada ya kujaza kuponi.
ILE Promosheni inayoendelea ya Bahati Nasibu ya Shinda Nyumba inayoendeshwa na Kampuni ya Global Publishers wachapishaji wa magazeti ya Champuioni, Uwazi, Risasi, Amani, Ijumaa na Ijumaa Wikienda leo imetua maeneo ya Vikindu-Mkuranga, Mkoa wa Pwani na kuchangamkiwa na wasomaji wengi ambao walinunua magazeti ya Uwazi.
Maofisa masoko wa Global Publishers,Yohana Mkanda na Jimmy Haroub waliwafikia wasomaji katika mitaa mbalimbali ya maeneo ya Vikindu Mkuranga ambapo waligawa zawadi za kofia zenye nembo iliyoandikwa ‘Shinda Nyumba’ baada ya washindi kununua Gazeti la Uwazi na kushiriki katika droo ya papo kwa papo waliyoiendesha.
“Droo kubwa mshindi atapata nyumba, lakini pia kuna zawadi nyingi ndogondogo zitakuwa zikitolewa, kwa mfano Alhamisi hii washindi wengi watakabidhiwa ving’amuzi vya TING na mwanamke mmoja, Lucy Swai wa Kibaha, Pwani, atakabidhiwa pikipiki yake, walishiriki kwa kununua magazeti la Global kwa shilingi 500 tu. Hivyo yeyote anaweza kushinda, jaribu leo na kesho,” alisema Mkanda.
Na Denis Mtima/Gpl