SIMANZI, majonzi vimetawala wakati wa kauagwa kwa mwili wa mama mzazi wa Mkurugenzi wa Makampuni ya Global Group, Eric Shigongo, Bi. Astreia Kahabi Kapela nyumbani kwake maeneo ya Mikocheni B, jijini Dar es Salaam leo Julai 29, 2018.
Bi. Asteriua Kapela alifariki dunia alfajiri ya Ijumaa, JulaiĀ 27 mwaka huu katika Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Muhimbili jijini Dar es Salaam alikokuwa amelazwa akipatiwa matibabu.
Baada ya kuagwa leo nyumbani kwake, mwili wa marehemu umepelekwa katika Kanisa Katoliki la Mt. Agatha lililopo Mikocheni B jijini Dar es Salaam kwa ajili ya iabada ya kumwombea marehemu kabla ya kusafirishwa kwenda jijini Mwanza kwa mazishi.
PICHA NA MUSA MATEJA | GLOBAL PUBLISHERS
Comments are closed.